Sunday, February 12, 2012

tabia ya kufanya mapenzi kwenye giza

Jamaa fulani alikuwa na tabia ya kufanya mapenzi kwenye giza na mkewe toka waoane...

Siku moja mkewe akaamua kuwasha taa kwa ghafla ili kujua ni kwa nn mumewe hapendi kufanya mapenzi na taa..

Ile kuwasha tuu akamkuta mumewe kashika "Vibrator" (kifaa alichokuwa anakitumia kufanya mapenzi na mkewe)...

Yule mwanamke akaondoka kwa hasira na kwenda kwao usiku ule ule, kesho yake akarudi na wazazi wake, pamoja na wazazi wa jamaa kwa ajili ya kusikiliza maelezo ya jamaa mbele ya familia nzima huku akifunguka...!!!!

MKE: "Mwanaume gani muongo wewe... Tena wewe pumbavu kabisa... Naomba unieleze sasa hivi ni kwanini umenidanganya miaka yote hiyo 20 ya ndoa?!"

MUME: "Samahanini wazazi wangu... Nakubali mimi ninaupungufu wa nguvu za kiume uliosababishwa na ajali niliyoipata mwezi mmoja baada ya ndoa yetu... Hiyo ilinifanya nisiweze fanya kitu kabisa kitandani, ndiyo maana nimekuwa namdanganya mke wangu miaka yote hiyokwa kutumia kifaa maalumu nilicho nunua Ulaya ili asiniache..."

Jamaa akanyanyuka, akaomba samahani, akatoka nje na kurudi na PANGA...

MUME: "Hayo yalikuwa ni maelezo yangu... Sasa naomba na wewe shetani unieleze, hao watoto saba wote uliowazaa umewatoa wapi??!!!"

No comments:

Post a Comment