Wednesday, March 28, 2012

mlenga shabaha, na mtaalam wa kuchuna ngoz



Jamaa wawili walikua marafiki saaaaaana wa damu..... Mmoja alikuwa mlenga shabaha, na mwengine mtaalam wa kuchuna ngozi!!! Wote walikuwa wanafanya kazi kama TEAM...

Siku moja wakaenda porini kuwinda, mtaalam wa kulenga shabaha akashuka kwenda mwituni kuwinda huku akimuacha mchunaji kwenye gari akimsubiri.... Ebwana daaaah!!!! Huku na kule mwituni mara ghafla jamaa si kakutana na SIMBA!!!!!

Duuuh, kifo noma... Jamaa akatoka nduki kama chizi, alipofika karibu na gari akamwambia mwenzake yule mtaalam wa kuchuna ngozi aliyebaki kwenye gari amfungulie mlango aingie... Jamaa akafungua mlango, ile anaruka tu kwenye gari mara jamaa si akajikwaa akadondoka wakat SIMBA naye alikuwa amesharuka...

Basi yule simba akapitiliza hadi ndani ya gari... Yaaaaaani faster baada tu ya yule simba kuzama kwenye gari yule muwindaji aliinuka faster na kufunga mlango wa gari huku akamwambia yule mtaalam wa kuchuna ngozi...

"Ebwana eeeh... We endelea kumchuna tuuu, wacha mi nikamtafute mwingine..."

No comments:

Post a Comment