Thursday, January 26, 2012

Chepe na Computer

Ebwana daaaaah!!!!! CHEPE alikuwa anamlalamikia rafiki yake kuwa Kiganja chake kinamuuma sana, inabidi akamuone daktari....

Rafiki yake akamjibu...
"Haina haja ya daktari.. Kuna computer mashine moja inaweza gundua tatizo lako na kukushauri haraka na kwa gharama nafuu zaidi ya kwa daktari...

Cha kufanya we beba kwenye kichupa kiasi kidogo cha haja ndogo na atakutatulia tatizo lako kwa 10,000/= tuu!!!"

Chepe kuona hivyo hakutaka poteza muda... Akabeba kiasi cha mkojo na kwenda kuonana na hiyo computer...

Baada ya kukabidhi, ile Computer ikaanza kuunguruma kwa dk. 1, ikabeep na kutoa kikaratasi cha majibu yake kilichosema....

**************************************
TATIZO:
-Unauvimbe ndani ya kiganja.
TIBA:
-Hakikisha unakanda kiganja chako na maji ya moto kila siku na epuka kukitumia hicho kiganja kwa kazi yoyote ile mpaka upone..
-Utapona ndani ya wiki moja!!
*************************************

Daaah, Chepe akatoka haamini hiyo technolojia mpya na jinsi inavyoweza fanya kazi... Akawaza na kusema...
"Haiwezekani... Siamini kabisa, ngoja niitegee mtego tuone kama ni kweli iko fit au utapeli tuu..."

Siku iliyofuata Chepe akaamua kumix maji ya bomba, mkojo wa mbwa wake, kiasi cha mkojo wa mke wake na wa mwanae... Akaona haitoshi akaamua kumasturbate humo humo ili kuikomoa ile Computer!!

Akaenda tena kwa ile Computer, akakabidhi pamoja na elfu kumi na kusubiri majibu... Computer kama kawaida ikanguruma dk. 1, ikabeep na kumpa majibu yake:

***************************************
TATIZO 1.
-Maji yako ya bomba si salama, ukinywa utapata kipindupindu.
TIBA
-Hakikisha unayachemsha kabla ya kunywa...

TATIZO 2.
-Mbwa wako anagonorrhea!!
TIBA
-Anza kumpa dawa ya ant-bacterium Neisseria!!

TATIZO 3.
-Mtoto wako anatumia cocaine na madawa mengine ya kulevya.
TIBA
-Mpeleke kwa washahuri nasaha kabla hajawa teja..

TATIZO 4.
-Mkeo anamimba, watoto mapacha!
TIBA
-Pole sana, Jiandae kulea mapacha ambao si wako!!

TATIZO 5.
-Kiganja chako kina uvimbe.
TIBA
-Usipoacha kumasturbate, hicho kiganja chako hakita pona KAMWE!!

NB: Ongeza hela kwa sababu nimetafiti sample tano, sample ya MAJI, MBWA, MKEO, MWANAO na WEWE. Jumla 50,000/=!!!!
************************************

***Copy write protected by Da Legendary Jason***

No comments:

Post a Comment